WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi ameingia lawamani kwa kudaiwa
kumlinda Mbunge wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM),
anayedaiwa kumbaka na kumtishia kumuua binti wa miaka 16.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi.
Akizungumza kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi wa simu (sms) na
Tanzania Daima jana, binti anayelalamika kutishiwa maisha na Profesa
Kapuya, amemtuhumu Waziri Nchimbi kushindwa kulishughulikia suala hilo
mapema licha ya kuwa na taarifa za tukio hilo muda mrefu.
Binti huyo alisema kuwa Dk. Nchimbi ni miongoni mwa mawaziri na viongozi
wa CCM waliokuwa wakifahamu kila kinachoendelea dhidi ya malalamiko
husika.
Alibainisha kuwa makada hao wa CCM walikuwa wakifanya jitihada za
kuhakikisha manyanyaso na vitisho kutoka kwa Profesa Kapuya haviwekwi
hadharani.
Katika kile kinachoonekana ni kukata tamaa juu ya usalama wake pamoja na
dada yake, binti huyo alisema amewasiliana na Waziri Nchimbi asubuhi ya
jana na kwamba waziri huyo hakuonyesha dalili yoyote ya kujali madhila
yao.
Alisema kutokana na Waziri Nchimbi kutokutilia uzito malalamiko yao,
waliamua kumuandikia ujumbe mfupi wa maandishi wakimshutumu kuendelea
kumlinda Profesa Kapuya.
“Nimemwambia katika ujumbe mfupi wa maneno (sms) kuwa jukumu la polisi
iliyo chini ya wizara yake ni kuhakikisha wananchi wanalindwa dhidi ya
manyanyaso na vitisho vya aina yoyote, na kwamba katika kadhia hii ya
Kapuya Jeshi la Polisi limekuwa kimya.
No comments:
Post a Comment